Jumanne, 2 Juni 2015

EL MERREIKH WAJIVUA KOMBE LA KAGAME, WASEMA HAWAWEZI KUJA KULITETEA DAR



MABINGWA watetezi wa mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame), El Merreikh ya Khartoum, Sudan imesema haitashiriki kutetea ubingwa wake wa michuano itakayofanyika kuanzia Julai 11 hadi Agosti 2 mwaka huu hapa nchini imefahamika.
Akizungumza na MANDELA MBEGEZE BLOG kutoka Khartoum, Ofisa Habari wa El Merreikh, Babiker Osman, alisema kwamba timu hiyo imeamua kujitoa kwenye mashindano ya Kombe la Kagame ni kutaka kuwekeza nguvu zaidi kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo Wasudan hao wameingia hatua ya makundi..

Osman alisema kuwa wanasikitika kuacha nafasi ya kutetea ubingwa wao na kuongeza kwamba wanaamini waandaaji wa michuano hiyo, Shirikisho la Soka la Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) wataelewa sababu zao za kujitoa kwenye michuano hiyo na wako tayari kushiriki kwenye michuano ya mwakani endapo watapata nafasi.

"El Merreikh haitashiriki Kombe la Kagame mwaka huu, sababu kubwa ni kujiandaa na mechi za makundi za mashindano ya Ligi ya Mabingwa, zitakuja timu nyingine kutoka Sudan", alisema Osman.
Alizitaja timu nyingine zitakazokuja kushiriki michuano hiyo kutoka Sudan ni Al Hilal ya Omdurman na Khartoum National ya Khartoum.
Baadhi ya timu nyingine zinazotarajiwa kushiriki mashindano hayo mwaka huu ni pamoja na Azam, Yanga, Simba zote za jijini Dar es Salaam, Gor Mahia (Kenya), KMKM (Zanzibar) na APR ya Rwanda.

El Merreikh ilifanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Kagame mwaka jana jijini Kigali, Rwanda kwa kuwafunga wenyeji APR bao 1-0 katika mchezo wa fainali uliofanyika kwenye Uwanja wa Amahoro mbele ya Mlezi wa Cecafa na Rais wa nchi hiyo, Paul Kagame.

Bingwa wa michuano hiyo inayofanyika kila mwaka hupata zawadi ya Dola za Marekani 30,000 wakati mshindi wa pili huondoka na Dola za Marekani 20,000 huku timu itakayomaliza ya tatu itajinyakulia Dola za Marekani 10,000.
Katika mashindano hayo mwaka jana Tanzania Bara iliwakilishwa na Azam baada ya Yanga iliyokuwa chini ya Mbrazil, Marcio Maximo ambayo ilipaswa kushiriki kujitoa.

Jumapili, 8 Februari 2015

ANGALIA BEKI HUYU ALIVYOKABA HADI SURA


 Mchezaji Robbie Neilson alijikuta kwenye maumivu makubwa baada ya kulambwa kiatu cha uso kutoka kwa nahodha wa timu ya Livingston, Jason Talbot.
Hiyo ilitokea wakati Livingston ikipambana na Hearts katika Ligi ya Scotland.
 Nicholson alilazimika kupata matibabu na kushonwa nyuzi kadhaa baada ya buti hilo la Talbot.
Walikuwa wanawania mpira wa juu, wakati Neilson akiruka kupiga kichwa, Tailbot alipeleka mguu na kumjeruhi vibaya.

KOCHA WA SIMBA ATUMA MAOMBI KWA MASHABIKI WA SIMBA


Kocha Mkuu wa Simba, Goran Kopunovic amesema kuna kila sababu ya mashabiki wa Simba kuendelea kumvumilia.


Amesema ana imani na kikosi chake kitakuwa na mabadiliko baada ya muda, lakini uvumilivu ndiyo dawa.
“Tumekuwa na vipindi vya kupanda na kushuka, utaona mechi moja tuko bora zaidi na nyingine tunashuka.

“Uvumilivu ndiyo jambo muhimu zaidi. Hatuwezi kufanikiwa kama leo tutachanganyikiwa na kuanza kufanya vitu nje ya msitari.
“Sare na Coastal si tulichokitaka, lakini angalau hatujapoteza mchezo tunaweza kuendelea kujipanga,” alisema Kopunovic raia wa Simba.

PLUIJM AWAPA DAWA WACHEZAJI WA YANGA KABLA YA KUIVAA YANGA LEO TAIFA



Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm amewaambia wachezaji wake, dawa ya kuondokana na kupoteza nafasi nyingi ni kuwa watulivu na kuachana na presha ya mashabiki kwa muda.


Pluijm raia wa Uholanzi, ameendelea kulizwa na wachezaji wake kupoteza nafasi za kufunga na kusema wanaweza kuzitumia vema kama wakijiondoa katika presha.

"Wachezaji wanachanganyikiwa kwa kuwa presha ni kubwa sana, wako wanataka kufunga kila mpira lakini wako ambao wanapata nafasi, lakini hawana utulivu.

"Yanga ni timu kubwa, presha ya mashabiki ipo juu na hii inawaathiri wachezaji.

"Nimezungumza nao mara kadhaa, nimesisitiza suala la presha na kuwaambia mashabiki wana haki yao katika kudai ushindi na mabao lakini wao wanapaswa kufanya kazi yao kwa ufasaha kwa mujibu wa tulichojifunza," alisema.

Yanga inashuka leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, kucheza mechi yake ya kwanza ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mtibwa Sugar.


SPURS YASHINDA DERBY YA LONDON





Harry Kane aliendelea kuimarika baada ya kuifunga Arsenal mabao mawili huku Tottenham ikitoka nyuma na kuibuka kidedea kwa mabao 2-1 katika mechi ya London Derby. Kane alifunga baada ya kupata pasi safi kutoka kwa Mousa Dembele aliyegusa krosi ya kona mapema katika kipindi cha pili. Baadaye alifunga kichwa kizuri katika dakika ya 86 na kuiweka Spurs juu ya Gunners katika jedwali la ligi ya Uingereza

 . Mesut Ozil aliiweka Arsenal kifua mbele katika kipindi cha kwanza laki mshambulizi yasio koma ya Tottenham katika ngome ya Arsenal yalizaa matunda na kuiweka Tottenham kuibuka kidedea.

CHELSEA YAONGOZA LIGI KWA POINTI SABA


 Kocha wa Chelsea Jose Mourinho amesema kwamba haoni uongozi wa alama 7 juu ya jedwali la ligi ya Uingereza ni fursa ya timu hiyo kushinda ligi hiyo mwaka huu. The Blues iliishinda Aston Villa 2-1 siku ya jumamosi huku Manchester City Inayoshikilia nafasi ya pili katika jedwali hilo ikiangukia sare ya 1-1 dhidi ya Hull City.

 James Milner alifunga bao la Mancity lakini hakuisaidia timu yake kupunguza pengo lililopo kati yake na Chelsea katika uongozi wa Ligi. Manchester city Hull City ilikuwa ya kwanza kufunga bao kupitia mchezaji David Meyler. Everton na Liverpool nazo zilitoka sare ya 0-0 katika Merseyside Derby iliochezwa katika uwanja wa Goodison Park Haya hapa baadhi ya matokeo ya mechi zilizochezwa jumamosi

. Tottenham 2 - 1 Arsenal Aston Villa 1 - 2 Chelsea Leicester 0 - 1 Crystal Palace Man City 1 - 1 Hull QPR 0 - 1 Southampton Swansea 1 - 1 Sunderland Everton 0 - 0 Liverpool

MSIMAMO WA LIGI YA BARA BAADA YA MICHEZO YA JANA

RnTimuPWDLFAGdPts
1Azam FC126421710722
2YANGA12642137622
3POLISI MORO144731211119
4JKT RUVU145451414019
5RUVU SHOOTING145451010019
6MTIBWA SUGAR11461137618
7Coastal Union14464109118
8KAGERA SUGAR144641111018
9SIMBA SC133821311217
10MBEYA CITY1344599016
11NDANDA FC144371218-615
12MGAMBO SHOOTING12426611-514
13STAND UNITED14266917-812
14T. PRISONS131841012-211